LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 23, 2017

KAMATI YA KUDUMU YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA KUTOKA BUNGE LA MSUMBIJI YATEMBELEA OFISI ZA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Chomera Jeremiah (kushoto) Ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa Rais, Wabunge na Madiwani mwaka 2015 wakati Kamati hiyo ilipotembelea Ofisi za Tume leo jijini Dar es salaam.


Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (katikati) akitoa ufafanuzi kuhusu majukumu ya Tume kwa  Wabunge wa Bunge la Msumbiji ambao ni Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa waliotembelea Ofisi za NEC jijini Dar es salaam kujifunza namna Tume hiyo inavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Lucas Chomera Jeremiah na Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Bw. Hamis Mkunga.




Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Emmanuel Kawishe (kushoto) akiwaeleza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji namna Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania inavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Chomera Jeremiah (kushoto) akifafanua jambo wakati wa kikao cha Wajumbe wa Kamati hiyo kutoka Msumbiji na watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania leo jijini Dar es salaam, Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji wamezitembelea Ofisi za NEC kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala ya Uchaguzi.Kulia ni Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji (R) Semistocles Kaijage.

 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (Kulia) akisalimiana na Wabunge wa Bunge la Msumbiji na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa wa nchi hiyo waliotembelea Ofisi za NEC kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu uendeshaji wa chaguzi mbalimbali.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) Jaji (R) Mhe. Semistocles Kaijage (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Utawala na Serikali za Mitaa ya Bunge la Msumbiji waliozitembelea Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi leo jijini Dar es salaam.  PICHA/Aron Msigwa - NEC

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages